MVUA ya mabaravu mfano wa mipira ya tofu usiku wa jana iliufanya mchezo wa kirafiki wa kimataifa baina ya Ubelgiji iliyoshinda 1-0 dhidi ya Tunisia usimame kwa muda..
Mchezo ulisimama dakika ya 40 kupisha hali hiyo na baada ya mambo kuwekwa saws uwanjani ukaendelea.
Lakini hali hiyo haikuizuia Ubelgiji kushinda, shukrani kwake mshambuliaji wa Chelsea, Romelu Lukaku aliyetokea benchi dakika ya 61 kuchukua nafasi ya kinda wa miaka 19, Divock Origi.
Mshambuliaji wa Manchester United, Adnan Januzaj alichea mechi yake ya kwanza rasmi ya kimataifa jana, wakati mshambuliaji mwingine wa Chelsea, Eden Hazard aliwakimbiza mno mabeki wa Tunisia.
Nikamateni kama mnaweza: Nyota wa Chelsea, Eden Hazard (kushoto) akiwatoka wachezaji wa Tunisia, wakiongozwa na Houcine Nater (kulia) jana
Mpira wa Kombe la Dunia mwaka huu, Brazuca ukiwa umezungukwa na mabarafu mfano wa mipira ya gofu uwanjani
0 comments:
Post a Comment